Kocha wa Al Ahly, Marcel Kohler, ameonyesha matumaini makubwa kuelekea mechi ya kesho dhidi ya Orlando Pirates, akisisitiza kuwa timu yake iko tayari kimwili na kiufundi. Emam Ashour ameonyesha utimamu wa hali ya juu mazoezini, na kikosi chote kimejipanga kwa changamoto hiyo. Ingawa Al Ahly haijawahi kushinda kwenye uwanja wa Orlando, Kohler anaamini kuwa mechi hii inaweza kuwa fursa yao ya kuandika historia mpya dhidi ya wapinzani wao wa Afrika Kusini. Mashabiki wanatarajia pambano lenye ushindani wa hali ya juu!