Vituo vya Usaili TRA kwa Watakaoitwa kwenye Interview Mamlaka ya Mapato Tanzania

Vituo vya Usaili TRA kwa Watakaoitwa kwenye Interview Mamlaka ya Mapato Tanzania Sehemu

Bonyeza hapo kujiunga nasi kupata matangazo mbalimbali ya kazi, Maswali ya Usaili.

Majina ya Usaili ajira za TRA kutoka kesho​

  • Vituo vya Usaili TRA kwa Watakaoitwa kwenye Interview Mamlaka ya Mapato Tanzania
Leo, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Moshi Jonathan Kabengwe amesema majina ya waombaji wa ajira 1,596 za TRA zilizotangazwa hivi karibuni yatatangazwa rasmi Machi 22.2025 kupitia tovuti ya tra.go.tz kwa ajili ya usaili wa kuandika utakaofanyika Machi 29 na 30 mwaka huu kwenye vituo 9.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam leo tarehe 21.03.2025 Bw. Kabengwe amesema kati ya waombaji 135,027 waliotuma maombi ya nafasi za ajira, waombaji 112,952 wamekidhi vigezo na kuitwa kwenye usaili wa kuandika.

Amesema kila muombaji atatumiwa taarifa ya kuitwa kwenye usaili katika barua pepe yake aliyoiambatanisha kwenye maombi ya kazi na kuwa waombaji wenye mahitaji maalum wamewekewa utaratibu maalum ambao utawasaidia kufanya usaili bila usumbufu.

Bw. Kabengwe amesema usaili huo utafanyika kwenye Mikoa 8 na Zanzibar ambayo ni

1. Dar es Salaam ambayo itahusisha waombaji kutoka Dar es Salaam na
Pwani.

2. Zanzibar ambayo itahusisha waombaji kutoka Unguja na Pemba

3. Arusha ambayo itahusisha waombaji kutoka Arusha, Manyara, Kilimanjaro na Tanga

4. Dodoma ambayo itahusisha waombaji kutoka Morogoro, Dodoma, Singida, Iringa na Tabora

5. Mtwara ambayo itahusisha waombaji kutoka Mtwara, Lindi na Ruvuma

6. Mbeya ambayo itahusisha waombaji kutoka Mbeya, Songwe na Rukwa

7. Mwanza ambayo itahusisha waombaji kutoka Mwanza, Shinyanga, Mara na Simiyu

8. Kagera ambayo itahusisha waombaji kutoka Kagera na Geita na

9. Kigoma ambayo itahusisha waombaji kutoka Kigoma na Katavi.
Vituo vya Usaili TRA kwa Watakaoitwa kwenye Interview Mamlaka ya Mapato Tanzania


Bw. Kabengwe amebainisha kuwa waombaji wote watatendewa haki.
 
Naomba msaada wa maswali ambayo wanauliza upande risk management officer II nimeomba nafasi hiyo TRA tauluma yangu ni Insurance risk management
 
Similar threads Most view View more
Hatua za Kuuliza swali. Anza na Title ya swali kisha Chini yake weka maelezo kuhusu swali lako.
Back
Top Bottom