GIZ ni shirika linalomilikiwa na serikali ya Shirikisho la Ujerumani, linalofanya kazi duniani kote kusaidia serikali ya Ujerumani kutimiza malengo yake katika ushirikiano wa kimataifa. Shirika hili hutoa huduma zenye tija, zinazolenga maendeleo endelevu kulingana na mahitaji ya wadau wake...