Christina Mwagala wa Tabora United Awachimba Yanga SC: "Wakiona Hawawezi, Waombe Mechi Irudiwe!"

Christina Mwagala wa Tabora United Awachimba Yanga SC: "Wakiona Hawawezi, Waombe Mechi Irudiwe!"

Haya hapa Matokeo ya Kidato cha Sita TUNDURU SECONDARY SCHOOL 2026-S0404 yaliyotangazwa na Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) Katika Mtihani wa Form six (ACSEE) 2026/2027 jumla ya wanafunzi wengi wamefaulu.
Bonyeza hapo juu kujiunge na Group la wanachuo waliomaliza kidato cha sita 2026 hapa baada ya matokeo ya form six 2026

Sia

Moderator

Staff member
Reputation: 100%
Joined
Oct 20, 2024
Messages
1,648
Christina Mwagala, Afisa Habari wa klabu ya Tabora United, ameonesha msimamo mkali dhidi ya Yanga SC baada ya mechi iliyochezwa jana. Katika mazungumzo yake na wanahabari, Christina alionyesha kutokujali kuhusu malalamiko ya Yanga SC akisema kuwa, kama wanaona hawakuridhishwa na matokeo, wana nafasi ya kuomba mchezo urudiwe.

"Kama Yanga wanaona wameonewa, waandike barua bodi ya ligi waombe hii mechi irudiwe. Wenyewe wachague wakitaka tukacheze Avic Town au hata juu mawinguni - popote wanapopataka tutawafunga vilevile kama hawajaridhika."
Christina aliongeza kwa kejeli kwamba hata kama Yanga SC wataomba mchezo urudiwe, Tabora United bado wako tayari kwa changamoto hiyo, na wana imani kuwa wataendeleza ushindi wao. "Kwa kuwa watu waliondoka wamenuna na kutoridhishwa, ni wakati wao kuomba mechi irudiwe. Turudiane, alafu tuwapige tena - tutawapiga sita badala ya tatu! Nyuki hakumbatiwi wala hapigwi busu!" alisema kwa kujiamini.

Tabora United Na Changamoto Kwa Yanga SC​

Christina Mwagala wa Tabora United Awachimba Yanga SC: Wakiona Hawawezi, Waombe Mechi Irudiwe!

Ushindi wa Tabora United umewafanya kuwa na ari na kujiamini zaidi, huku wakisubiria majibu kutoka kwa Yanga SC iwapo wataamua kuchukua hatua yoyote rasmi. Kauli za Christina zinaashiria kuwa klabu hiyo ya Tabora haijaridhika tu na matokeo, bali pia iko tayari kwa ushindani wowote endapo Yanga SC wataomba mchezo urudiwe.

Mashabiki Na Wakosoaji Wa Maamuzi Ya Mechi​

Baada ya mechi hiyo, mashabiki wa timu zote wameonekana kugawanyika, huku baadhi wakiamini kuwa maamuzi yalikuwa sahihi na wengine wakihoji baadhi ya maamuzi ya waamuzi wa mchezo. Hata hivyo, Tabora United wanaonekana kutokuwa na wasiwasi wowote kuhusu maamuzi hayo, wakisisitiza kuwa ushindi wao ulikuwa wa haki.

Je, Yanga SC watachukua hatua za kisheria au watakubali matokeo kama yalivyo?
 
Similar content Most view View more
Back
Top Bottom