WITO WA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA JKT MUJIBU WA SHERIA MWAKА 2025

WITO WA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA JKT MUJIBU WA SHERIA MWAKА 2025 Waliochaguliwa JKT 2

Bonyeza hapo kujiunga nasi kupata matangazo mbalimbali ya kazi, Maswali ya Usaili.
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Meja Jenerali Rajabu Nduku Mabele, anatoa wito kwa Vijana waliohitimu elimu ya sekondari kidato cha sita kwa mwaka 2025, kutoka Shule zote za Tanzania Bara kuhudhuria Mafunzo ya JKT kwa Mujibu wa Sheria kwa mwaka 2025.

Sanjari na wito huo, JKT limewapangia makambi watakayo kwenda kupatiwa Mafunzo na wanatakiwa kuripoti makambini kuanzia tarehe 28 Mei 2025 tarehe hadi 08 Juni 2025.

Vijana hao wamepangwa katika Kambi za JKT zifuatazo; JKT Rwamkoma - Mara, JKT Msange - Tabora, JKT Ruvu na JKT Kibiti - Pwani, JKT Mpwapwa, JKT Makutupora - Dodoma, JKT Mafinga - Iringa, JKT Mlale - Ruvuma, JKT Mgambo na JKT Maramba -Tanga, JKT Makuyuni na JKT Orjolo - Arusha, JKT Bulombora, JKT Kanembwa na JKT Mtabila - Kigoma, JKT Itaka - Songwe, JKT Luwa na JKT Milundikwa - Rukwa pamoja na JKT Nachingwea - Lindi.

Wahitimu wenye ulemavu wa kuonekana kwa macho (Physical Disabilities) waripoti katika Kambi ya Ruvu JKT iliyopo Mlandizi Mkoani Pwani ambayo ina miundombinu ya kuhudumia watu wa jamii hiyo.

Pakua majina ya waliochaguliwa JKT 2025 hapa.
WITO WA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA JKT MUJIBU WA SHERIA MWAKА 2025
 
Hatua za Kuuliza swali. Anza na Title ya swali kisha Chini yake weka maelezo kuhusu swali lako.
Back
Top Bottom