Huu hapa Mfumo wa Maombi ya Vyuo Udahili wa Pamoja (CAS) 2025 Tangazo la Kujiunga na Vyuo vya Afya na Sayansi Shirikishi kwa Mwaka wa Masomo 2025/2026 Mwisho wa Kutuma Maombi ya Mzunguko wa Kwanza: Tarehe 11/07/2025.
Mambo Muhimu ya Kuzingatia:
tvetims.nacte.go.tz
Mambo Muhimu ya Kuzingatia:
- Hakikisha unatumia barua pepe (email) inayofanya kazi na namba ya simu ambayo inatumika.
- Chagua kozi unayoipendelea kulingana na sifa zako.
- Unaweza kuchagua hadi vyuo/programu 12 kwa wakati mmoja.
- Ada ya maombi ni Tsh 15,000 kwa chuo kimoja na ukomo ni Tsh 45,000 kwa vyuo/programu zote (ada haitarudishwa).
- Utapewa namba ya malipo (Control Number) baada ya kujaza maombi.
- Malipo yanaweza kufanyika kwa Tigo Pesa, M-Pesa, Airtel Money au benki.
- Kabla hujachagua kozi yoyote, soma Mwongozo wa Uandikishaji kujua sifa zinazohitajika kwa kila programu.
CAS | Central Admission System