Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) linapenda kuutaarifu umma kuwa udahili wa wanafunzi katika ngazi ya Astashahada na Stashahada kwa muhula wa Machi, 2025 utaanza rasmi tarehe 10 hadi 28 Februari, 2025. Udahili huu unahusisha vyuo vyote vilivyoidhinishwa na vyenye nafasi za kupokea wanafunzi wapya, isipokuwa vyuo vya afya kwa Tanzania Bara. Hii ni fursa muhimu kwa wahitimu wa elimu ya sekondari na wale waliomaliza mafunzo katika vyuo mbalimbali kuendelea na safari yao ya kitaaluma katika taasisi zilizoidhinishwa na Baraza.
Wahitimu wote wenye sifa za kujiunga na kozi za Astashahada na Stashahada wanahimizwa kutuma maombi yao moja kwa moja kwenye vyuo wanavyovipenda. Baada ya mchakato wa uchaguzi kufanyika, majina ya wanafunzi waliodahiliwa yatapelekwa NACTVET kwa ajili ya uhakiki wa mwisho kabla ya kuruhusiwa kujiunga na masomo. Ni muhimu kwa waombaji kuhakikisha kuwa wanakamilisha taratibu zote za udahili kwa usahihi na kwa wakati ili kuepuka changamoto zisizo za lazima. Masomo kwa wanafunzi waliokamilisha hatua zote za udahili yataanza rasmi tarehe 07 Aprili, 2025.
Vyuo vyote vinavyodahili wanafunzi kwa muhula huu vinasisitizwa kufuata taratibu na miongozo iliyowekwa na NACTVET, ikiwa ni pamoja na kuzingatia Kalenda ya Udahili (Admission Calendar) inayopatikana kwenye tovuti rasmi ya Baraza. Kufuatwa kwa taratibu hizi kunasaidia kuhakikisha kuwa mchakato wa udahili unakuwa wa haki, uwazi, na wenye viwango vinavyotakiwa ili kulinda ubora wa elimu na mafunzo ya ufundi nchini.
Baraza linatoa wito kwa waombaji na wazazi kuwa makini katika kuchagua vyuo kwa kuhakikisha wanajiunga na taasisi zilizoidhinishwa kufanya udahili wa Machi, 2025. Orodha rasmi ya vyuo vilivyoruhusiwa kufanya udahili kwa muhula huu inapatikana kwenye tangazo hili na pia kwenye tovuti rasmi ya NACTVET kupitia www.nactvet.go.tz. Waombaji wanahimizwa kujielimisha zaidi kuhusu programu mbalimbali zinazotolewa ili kufanya maamuzi sahihi kwa mustakabali wa taaluma na ajira zao za baadaye.
Pakua tangazo la udahili wa masomo vyuo mbalimbali hapa
Wahitimu wote wenye sifa za kujiunga na kozi za Astashahada na Stashahada wanahimizwa kutuma maombi yao moja kwa moja kwenye vyuo wanavyovipenda. Baada ya mchakato wa uchaguzi kufanyika, majina ya wanafunzi waliodahiliwa yatapelekwa NACTVET kwa ajili ya uhakiki wa mwisho kabla ya kuruhusiwa kujiunga na masomo. Ni muhimu kwa waombaji kuhakikisha kuwa wanakamilisha taratibu zote za udahili kwa usahihi na kwa wakati ili kuepuka changamoto zisizo za lazima. Masomo kwa wanafunzi waliokamilisha hatua zote za udahili yataanza rasmi tarehe 07 Aprili, 2025.
Vyuo vyote vinavyodahili wanafunzi kwa muhula huu vinasisitizwa kufuata taratibu na miongozo iliyowekwa na NACTVET, ikiwa ni pamoja na kuzingatia Kalenda ya Udahili (Admission Calendar) inayopatikana kwenye tovuti rasmi ya Baraza. Kufuatwa kwa taratibu hizi kunasaidia kuhakikisha kuwa mchakato wa udahili unakuwa wa haki, uwazi, na wenye viwango vinavyotakiwa ili kulinda ubora wa elimu na mafunzo ya ufundi nchini.
Baraza linatoa wito kwa waombaji na wazazi kuwa makini katika kuchagua vyuo kwa kuhakikisha wanajiunga na taasisi zilizoidhinishwa kufanya udahili wa Machi, 2025. Orodha rasmi ya vyuo vilivyoruhusiwa kufanya udahili kwa muhula huu inapatikana kwenye tangazo hili na pia kwenye tovuti rasmi ya NACTVET kupitia www.nactvet.go.tz. Waombaji wanahimizwa kujielimisha zaidi kuhusu programu mbalimbali zinazotolewa ili kufanya maamuzi sahihi kwa mustakabali wa taaluma na ajira zao za baadaye.
Pakua tangazo la udahili wa masomo vyuo mbalimbali hapa
Nafasi za Masomo Chuo cha CBE March 2025
Ada, Sifa, Vigezo