Viingilio vya Yanga SC vs. Al Hilal: Mechi Kubwa, Ligi ya Mabingwa 2024/2025 | Tiketi Zaanza Kuuzwa Rasmi!

Habari za Michezo Viingilio vya Yanga SC vs. Al Hilal: Mechi Kubwa, Ligi ya Mabingwa 2024/2025 | Tiketi Zaanza Kuuzwa Rasmi!

Bonyeza hapo kujiunga nasi kupata matangazo mbalimbali ya kazi, Maswali ya Usaili.
Hatua za Kuuliza swali. Anza na Title ya swali kisha Chini yake weka maelezo kuhusu swali lako.

GiftVerified member

Administrator

Staff member
Reputation: 100%
Joined
Oct 19, 2024
Messages
1,180
Hivi hapa Viingilio vya Yanga SC vs. Al Hilal: Mechi Kubwa, Ligi ya Mabingwa Yanga SC 2024/2025 | Tiketi Zaanza Kuuzwa Rasmi! Wananchi, mchezo wetu dhidi ya Al Hilal unakaribia! Mechi hii muhimu itachezwa tarehe 26 Novemba 2024, kuanzia saa 10:00 jioni, kwenye uwanja wetu wa kihistoria, Benjamin Mkapa Stadium.

Viingilio vya Yanga SC vs Al Hilal​

Ili kuhakikisha kila mmoja anapata nafasi ya kushuhudia tukio hili kubwa, viingilio vimepangwa kwa bei nafuu kama ifuatavyo:
Viingilio vya Yanga SC vs. Al Hilal: Mechi Kubwa, Ligi ya Mabingwa 2024/2025 | Tiketi Zaanza Kuuzwa Rasmi!

  • VIP A: TSh 30,000
  • VIP B: TSh 20,000
  • VIP C: TSh 10,000
  • Machungwa na Mzunguko: TSh 3,000
Tiketi za mchezo huu tayari zipo sokoni! Unaweza kununua tiketi yako kupitia njia zifuatazo:
  1. Makao Makuu ya Klabu, Jangwani – Njoo ujihakikishie tiketi mapema.
  2. Mitandao ya Simu – Urahisi wa kupata tiketi kwa njia ya kidigitali, bila foleni.
  3. Vituo Maalum – Orodha ya vituo itatangazwa kwenye kurasa rasmi za mitandao yetu ya kijamii leo.
Kwanini Uhudhurie?
  • Mchezo huu si wa kukosa! Ni nafasi yetu kuonyesha mshikamano kama Wananchi na kutoa sapoti ya nguvu kwa wachezaji wetu.
  • Kwa mashabiki waliofika uwanjani, watapata fursa ya kipekee kushuhudia ubora wa kikosi kipya cha Yanga SC chini ya uongozi wa kocha wetu mpya.
  • Uwanja wa Benjamin Mkapa uwe mahali pa sauti moja ya kuwatia hamasa wachezaji wetu na kuhakikisha ushindi dhidi ya wapinzani wetu.
Wananchi, tujitokeze kwa wingi na kuhakikisha tunakuwa sehemu ya historia nyingine ya Yanga SC. Timu yetu inatutegemea – hakikisha tiketi yako leo! 💚💛
 
Similar threads Most view View more
Back
Top Bottom