Habari wanajukwaa,
Naomba msaada wa ufafanuzi au uzoefu kwa yeyote aliyewahi kupitia utaratibu wa kuomba nafasi ya internship kwenye Taasisi X ( ya Serikali) kupitia TAESA.
Niliwasiliana na Taasisi X kuhusiana na nafasi za internship, lakini walieleza kuwa wao hawapokei maombi moja kwa moja, bali wanapokea kupitia TaESA. Hivyo walinishauri nitume maombi kupitia taasisi hiyo
Tangu nifanye hivyo, sijapata mrejesho wowote kutoka TAESA licha ya kufuatilia kwa muda sasa kupitia mawasiliano mbalimbali, ikiwemo kutuma barua pepe na ujumbe wa WhatsApp kwa wahusika waliotajwa.
Maswali yangu:
1. Je, ni utaratibu wa kawaida kuchelewa kupata mrejesho kutoka TAESA?
2. Kuna anayefahamu njia mbadala au hatua ya kuchukua ili kufanikisha zoezi hili?
3. Ikiwa Taasisi X hawajasema moja kwa moja kuwa nafasi ipo, je bado ni sahihi kuendelea kusubiri kupitia TAESA?
Naomba msaada wenu kwa yeyote aliye na taarifa sahihi au aliyepitia hali kama hii.
Ahsanteni.
Naomba msaada wa ufafanuzi au uzoefu kwa yeyote aliyewahi kupitia utaratibu wa kuomba nafasi ya internship kwenye Taasisi X ( ya Serikali) kupitia TAESA.
Niliwasiliana na Taasisi X kuhusiana na nafasi za internship, lakini walieleza kuwa wao hawapokei maombi moja kwa moja, bali wanapokea kupitia TaESA. Hivyo walinishauri nitume maombi kupitia taasisi hiyo
Tangu nifanye hivyo, sijapata mrejesho wowote kutoka TAESA licha ya kufuatilia kwa muda sasa kupitia mawasiliano mbalimbali, ikiwemo kutuma barua pepe na ujumbe wa WhatsApp kwa wahusika waliotajwa.
Maswali yangu:
1. Je, ni utaratibu wa kawaida kuchelewa kupata mrejesho kutoka TAESA?
2. Kuna anayefahamu njia mbadala au hatua ya kuchukua ili kufanikisha zoezi hili?
3. Ikiwa Taasisi X hawajasema moja kwa moja kuwa nafasi ipo, je bado ni sahihi kuendelea kusubiri kupitia TAESA?
Naomba msaada wenu kwa yeyote aliye na taarifa sahihi au aliyepitia hali kama hii.
Ahsanteni.