JOSHUA MUTALE (BUDO) MBIONI KUONDOKA MSIMBAZI

JOSHUA MUTALE (BUDO) MBIONI KUONDOKA MSIMBAZI

Orodha ya majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano au Jinsi ya kuangalia selection za form six selection 2026 Tamisemi
Bonyeza hapo juu kujiunge na Group la Form Six Selection 2026 hapa

Revoo

Member

Reputation: 22%
Joined
Dec 12, 2024
Messages
194
TOFAUTI na matarajio ya viongozi na hata mashabiki na wapenzi wa Simba wakati anasajiliwa, ukweli ni kwamba Mzambia Joshua Mutale anahesabu siku tangu dirisha dogo la usajili likifunguliwa leo, kutokana na kinachoelezwa majeraha ya mara kwa mara yanaweza kumng’oa Msimbazi.
FB_IMG_1734261251458.webp


Mutale alisajiliwa kwa mbwembwe katika dirisha kubwa la msimu huu, lakini ameshindwa kufanya maajabu akiwa hana bao lolote katika Ligi Kuu, kitu kinachoelezwa kimewafanya mabosi wa klabu hiyo kufikiria kumpiga chini ili nafasi yake aletwe mtu wa maana wa kuisaidia timu hiyo inayosaka heshima baada ya misimu mitatu mfululizo kushindwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu na Kombe la Shirikisho.

Mutale alijiunga na Simba kwa mkataba wa miaka mitatu akitokea Power Dynamos ya Zambia Hadi sasa hana mwendelezo wa kucheza mara kwa mara kutokana na majeraha ya mara kwa mara.
 
Similar content Most view View more
Back
Top Bottom